IMEKAA poa sana! Mkongwe kwenye anga la sinema za Kibongo, Salome Urassa 'Thea' amekula kiapo cha aina yake kwamba siku akionekana amejichubua na kuondoa rangi yangi yake nyeusi ya asili, asulubiwe mchana kweupe.

Mkongwe kwenye anga la sinema za Kibongo, Salome Urassa 'Thea'.
Thea aliliambia gazeti hili kuwa hakuna kitu anachopenda kwenye mwili wake kama ngozi yake na hata siku moja hajawahi kupata ushawishi wowote wa kuharibu ngozi yake na anawaonea huruma mastaa waliotumia mkorogo.
“Nasema kabisa kutoka moyoni, kama kweli itatokea siku nikajichubua, naombeni kabisa mnisulubishe maana napenda ngozi yangu kuliko kitu chochote,” alisema Thea.
Thea aliliambia gazeti hili kuwa hakuna kitu anachopenda kwenye mwili wake kama ngozi yake na hata siku moja hajawahi kupata ushawishi wowote wa kuharibu ngozi yake na anawaonea huruma mastaa waliotumia mkorogo.
“Nasema kabisa kutoka moyoni, kama kweli itatokea siku nikajichubua, naombeni kabisa mnisulubishe maana napenda ngozi yangu kuliko kitu chochote,” alisema Thea.