
Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Shariff Hamad na umoja wa UKAWA leo wamewatembelea na kuwapa pole ndugu wa marehemu waliofariki kwenye ajali ya moto hapo jana maeneo ya Buguruni Malapa.
Baba wa Familia iliyoteketea kwa moto (Masoud) amesema majina ya marehemu yalikuwa ni Samira Juma ambaye alikuwa mke wake. Ahmed Masoud, Aisha Masoud , Abilah masoud, Ashraf Masoud, hawa walikuwa watoto wake, mama yake mzazi, mfanyakazi wa ndani, na mwanamke aliyejukana kwa jina la Wadh hat akiwa na mtoto wake mdogo wa mwaka mmoja na nusu.

Baadhi ya picha zikionesha nyumba iliyoungua na sehemu waliyozikwa jana wale watu 9 wa familia moja wakiwemo watoto watano waliofariki kwa moto baada ya nyumba yao kuungua moto na wao kuungulia ndani eneo la Buguruni Malapa, Ilala jijini Dare es salaam.






