Hii inakuwa kolabo ya pili kati ya Ommy Dimpoz na Alikiba baada ya miaka minne. Alikiba yuko chini ya usimamizi wa Studio ya Kimataifa ya ROCKSTAR4000 na Rockstar Publishing wakati Ommy Dimpoz yuko chini ya PKP Management.
Wimbo huu uliobeba ujumbe wa mapenzi unazungumzia mwanamke wa ndoto zao uliandikwa na Ommy Dimpoz pamoja na Alikiba na kufanyiwa kazi na mtayarishaji Emmma The Boy. Video pia iko tayari katika chaneli ya YouTube ya AliKiba na unaweza kuitizama hapo chini. Pakua : http://bit.ly/Kajiandae kisha tupe mrejesho wako.