Quantcast
Channel: DUNIA KIGANJANI BLOG | Ifanye Dunia Kuwa Yako
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2674

Jeshi La Polisi Shinyanga Kumaliza Vitendo Vya Uhalifu Mkoani Humo Na Kutoa Zawadi Ya Mfanyakazi Bora Wa Jeshi Hilo Kila Mwisho Wa Mwezi

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga limeanzisha utaratibu wa kila mwezi kubaini askari mfanyakazi bora, na kumpa zawadi huku anayefanya kazi vibaya kumchukulia hatua ili kuleta ufanisi katika jeshi hilo, na kuhakikisha vitendo vya kihalifu vimekwisha mkoani humo.

Hayo yamesemwa jana na Kamanda mpya wa Jeshi hilo mkoani humo ACP MULIRO JUMANNE MULIRO mjini Shinyanga alipokutana na waandishi wa habari mkoani humo kwa lengo la kujitambulisha.

Akielezea baadhi ya mikakati yake Muliro amesema hatakuwa tayari kufanyakazi na askari wanaobambikizia watu wasio na hatia kesi kwa lengo la kujipatia rushwa na atahakikisha upelelezi wa mashauri yote unakamilika kwa muda mfupi.

Muliro ametaka askakri polisi kutenda haki, kuepuka matumizi ya lugha chafu na vitendo vya rushwa ambavyo vimekuwa vikilitia doa jeshi la polisi na kwamba tathmini ya mambo hayo itafanyika kila mwezi.

Amesema atahakikisha analiongoza jeshi hilo kwa weledi akishikisha wananchi pamoja na vyombo vya habari katika kufukia malengo hayo.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2674

Trending Articles